395px

Sitaki Tena

Phina

Nitachowaambia msiache kumwambia na yeye
Simchukii na, na najipa mweyewe oh, no
oh, baby sijutiii kuwa mbali naye apunguze presha
Mwambieni sililii, penzi lake nilishalihimisha

Hazijabaki memory wala kumbukumbu
Nilishamsahau mazima
Hata nikimwona namwona ka nungu nungu
Sio kama namvunjia heshima
Makombe amalize ajifushe na nyungu
Akakoge na maji ya kisima
Ila mimi nilisha apa kwa mwenyezi Mungu
Haitojirudia daima

Sitaki tena, tena mwambieni asinisumbue mimi
Sitaki tena, nipo buheri na nafsi yangu
Sitaki tena, abaki na zake nibaki na zangu
Sitaki tena, nipo buheri na nafsi yangu

Dua zake mbaya kwangu nifeli nilipo sasa anajua
Najua likiwa ka kiza kikitanda ananiwaza ananijua
Mwambieni asihangaike na mipasho moyo wake mimi naujua
Sitaki kumdhalilisha nikataja na siri zake nikaamuumbua

Hazijabaki memory wala kumbukumbu
Nilishamsahau mazima
Hata nikimwona namwona ka nungu nungu
Sio kama namvunjia heshima
Makombe amalize ajifushe na nyungu
Akakoge na maji ya kisima
Ila mimi nilisha apa kwa mwenyezi Mungu
Haitojirudia daima

Sitaki tena, tena mwambieni asinisumbue mimi
Sitaki tena, nipo buheri na nafsi yangu
Sitaki tena, abaki na zake nibaki na zangu
Sitaki tena, nipo buheri na nafsi yangu

Mwambieni sijutiii kuwa mbali naye apunguze presha
Mwambieni sililii, penzi lake nilishalihimisha

Composição: