Kijuso (feat. Rayvanny)
Queen Darleen
Eyoo Laizer
Wasafi Records
Unaringa kitu gani, we mwenyewe ujisute
Afadhali hata nyani, sio we mwanamke!
Hupendezi asilani, sio unyoe, usuke
Nilifata kitu gani? Umefanya nijute!
Mi nakuona punguwani, na usikurupuke
Kwanza naongea na nani? Naomba nikumbushe
Mi nawe hatuendani, jipandishe jishushe!
Usinipande kichwani, namba yangu ifute
Hizo dharau, mwana mvyoro papu
Naona unasahau nyuzi zako nilikapu
Nimepanda dau, mkataba nimekata
Tena nyang'au, ndo ukome kunifata
Unaringa una nini? Kijuso!
Vijimeno kama jini, Gaucho!
Kwani nawe una nini? Kituko!
Usio na kazi mjini, popo!
Punguza kelele
Acha kelele mama
Punguza kelele baba
Acha kelele bwana
Eti nawe unavimba, perfume tu mtihani!
Kwanza shirt ulovaa umeazima kwa nanii
Wanifata kapuku, utanipa nini?
Nilikuacha, leo kimekuwasha nini?
Funga bakuli mbele yangu we mshamba
Nakujua vizuri toka unavaa mabwanga
Kati unanuka moshi, huna hata ishu!
Kwenye pochi wanja na tishu
Unapenda ganda la ndizi, kuteleza
Wakati kupambana mpaka mchuzi wa pweza!
Dume zima tantara tantara
Instagram ina hue
Wakati kwenu kula, kulala, huchangii hata kitunguu
Hizo dharau, mwana mvyoro papu
Naona unasahau nyuzi zako nilikapu
Nimepanda dau, mkataba nimekata
Tena nyang'au, ndo ukome kunifata
Unaringa una nini? Kijuso!
Vijimeno kama jini, Gaucho!
Kwani nawe una nini? Kituko!
Usio na kazi mjini, popo!
Punguza kelele
Acha kelele mama
Punguza kelele baba
Acha kelele bwana



Comentários
Envie dúvidas, explicações e curiosidades sobre a letra
Faça parte dessa comunidade
Tire dúvidas sobre idiomas, interaja com outros fãs de Queen Darleen e vá além da letra da música.
Conheça o Letras AcademyConfira nosso guia de uso para deixar comentários.
Enviar para a central de dúvidas?
Dúvidas enviadas podem receber respostas de professores e alunos da plataforma.
Fixe este conteúdo com a aula: